Thursday, July 10, 2014

Benki Kuu ya Tanzania yazungumzia uanzishwaji wa sarafu ya Shilingi 500 na sababu za uamuzi huo

Benki Kuu ya Tanzania yazungumzia uanzishwaji wa sarafu ya Shilingi 500 na sababu za uamuzi huo
Akizungumza katika kipindi chakili break fast show, Meneja wa huduma za kibenki toka Benki Kuu ya Tanzania, Emmanuel Boaz amesema wameamua kubadili matumizi ya noti ya shilingi 500 na kutumia sarafu kwa kuwa noti hiyo inachakaa haraka na mzunguko wake ni mkubwa sana kiasi kwamba hairudi benki.
“Noti ya shilingi 500 kwa wasitani hushikwa na watu zaidi ya milioni moja kwa siku. Na kwa wasitani tunaweza kusema noti moja hushikwa na watu 20 hadi 25 kwa siku. Huo ni mzunguko mkubwa ukilinganisha na idadi ya watu wanaoshika noti ya shilingi 10,000. ” Amesema Emmanuel Boaz.
“Na ukizingatia watu wengi wanaoishika noti hii ni wale wenye matumizi ya kawaida ya nyumbani ambao wengi wao sio wanaopeleka benki, hivyo noti hii kwa kiasi kikubwa hairudi benki, labda wanaorudisha benki ni taasisi kama makanisa, misikiti n.k” Ameongeza.
Boaz amewatoa wasiwasi watanzania ambao wanadhani matumizi ya sarafu hiyo yataleta madhara hasi kwa uchumi wa Taifa na kueleza kuwa hakutakuwa na athari yoyote na kwamba tofauti na noti sarafu hiyo ina uwezo wa kudumu kwa zaidi ya miaka 20.
Sarafu hiyo itakayoanza kutumika rasmi miezi miwili au mitatu ijayo ina taswira ya rais wa kwanza wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sheikh Amani Abeid Karume.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...