Thursday, July 10, 2014

Majanga: Albam aliyomuimbia mkewe yauza nakala 530 tu Uingereza wiki ya kwanza

Majanga: Albam aliyomuimbia mkewe yauza nakala 530 tu Uingereza wiki ya kwanza
Muimbaji Robin Thicke anazidi kukutwa na majanga zaidi baada ya kumsaliti mkewe Paul,  kosa lililopelekea kutoswa na mke wake. Sasa albam nzima aliyoiimba kwa ajili ya kumuomba msamaha na kumbembeleza mkewe imebuma kwa mauzo.
Albam ya ‘Paula’ inaripotiwa kuuza nakala 530 tu katika wiki yake ya kwanza nchini Uingereza, huku Canada ikiwa imeuza nakala 550 tu katika wiki yake ya kwanza. Marekani imeuza Units 24, 000.
Mauzo hayo yatazidi kumsononesha Robin Thicke ambaye alikuwa akizunguka kwenye matamasha akimuomba msamaha mkewe jukwaani mara kwa mara, huenda watu wamechoka kusikia kilio chake kuhusu mkewe.
Mauzo ya Paula ni tofauti kabisa na mauzo ya albam yake ya  Blurred Lines ambayo iliuza nakala 177,000 katika wii ya kwanza Marekani huku ikishika nafasi ya kwaza Uingereza.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...