Thursday, July 10, 2014

Picha: Angelina Jolie alikuwa mtumiaji wa dawa za kulevya! Aliyekuwa akimuuzia asimulia

Picha: Angelina Jolie alikuwa mtumiaji wa dawa za kulevya! Aliyekuwa akimuuzia asimulia
Wiki iliyopita kuna video inayomuonesha muigizaji maarufu wa kike, Angelina Jolie akiwa anaongea na simu kwenye chumba kichafu au tunaweza kusema kina mazingira ya ajabu, video ambayo walipewa National Enquirer na mfanyabiashara wa madawa ya kulevya aliyefungwa, Franlin Meyaer.
Mayer anadai kuwa alishuti kipande cha dakika 16 kwa kuruhusiwa na Angelina Jolie mwaka 1999 katika nyumba yake ya Manhattan kumuuzia madawa aina ya heroin na Cocaine.“Angie ni mteja wangu wa miaka mingi. Nilikuwa namuuzia heroine na cocaine. Siku moja lainiita nyumbani kwake. Hiyo ndiyo ilikuwa njia ya kuniambia kuwa anataka nimpelekee mzigo (dawa za kulevya). Kwa muda huo nilikuwa nimenunua video camera na nikaamua kwenda nayo. Na nilipofika nilimpa dawa za kulevya na yeye akanipa pesa yangu. Alionekana kutojali nani alikuwa pale.” Ameeele Mayer.
Maelezo ya bwana Mayer yanashabihiana na maelezo ya Angelina Jolie ya mwaka 2011 ambapo aliwahi kukaririwa akizungumzia mambo magumu aliyowahi kuyapitia kabla hajawa mtu anaeheshimika zaidi sasa hivi na mfano wa kuigwa kwa wanawake na jamii kwa ujumla.
“Nilipitia wakati wa mgumu, wakati wa kiza na nikavuka. Sikufa nikiwa kijana, kwa hiyo nina bahati sana. Kuna wasanii wengine na watu abao wahawakuweza kuvishinda vitu hivyo. Nadhani watu wanaweza kuimagine kwamba nilifanya vitu hatari zaidi na vichafu zaidi. Kwa sababu mbalimbali nisingeweza kuwa hapa. Unafikiria kuhusu hayo pia mara nyingi wakati unapokuwa karibu na vitu vingi hatari, na nafasi nyingi zimechukuliwa mbali zaidi.”Alisema Angelina Jolie
Hayo yalikuwa ya zamani, hivi sasa Angie ni muigizaji anaesaidia sana jamii hasa wasichana wa Afrika na amejenga mashule na kutoa misaada mbalimbali kusaidia kutokomeza udhalilishaji na unyanyasaji.
Ni mama hodari wa familia yake na muigizaji Brad Pitt.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...