Thursday, July 10, 2014

UN: Umasikini S/Kusini umesababishwa na serikali, waasi

UN: Umasikini S/Kusini umesababishwa na serikali, waasiMkuu wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa huko Sudan Kusini amesema kuwa viongozi wa serikali wanaohudumia maslahi yao binafsi na waasi ndio sababu ya njaa "iliyotengenezwa na mwanadamu" nchini humo.
Hilde Johnson anayeongoza ujumbe wa Umoja wa Mataifa huko Sudan Kusini ameikemea serikali ya Juba la waasi kwa nafasi yao katika kuitumbukiza hatarini zaidi Sudan Kusini ambayo amesema ni miongoni wma nchi maskini zaidi duniani. Amesema maelfu ya watu wameuawa nchini humo na kutahadharisha kwamba nchi hiyo sasa imerudi nyuma kwa miongo kadhaa. Jonson amesema kuwa saratani ya ufisadi wa mabilioni ya dola yanayotokana na mafuta imewakumba viongozi wa nchi hiyo na kuwasababishia laana. Hilde Johnson ameyasema hayo katika maadhimisho ya mwaka wa tatu wa kutangazwa uhuru na kujitawala Sudan Kusini.
Maelfu ya watu wameuawa nchini Sudan Kusini na wengine zaidi ya milioni 1.3 kufukuzwa katika makazi yao kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya jeshi la serikali na waasi wanaoongozwa na makamu wa zamani wa rais wa Sudan Kusini. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon pia amezitaka pande mbili hasimu nchini humo kurejea katika meza ya mazungumzo ya amani.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...