Tuesday, June 24, 2014

China yaongoza katika biashara ya rejereja kupitia mtandao wa Internet


Thamani ya soko la biashara ya rejareja kupitia mtandao wa Internet nchini China ilifikia dola bilioni 296 za kimarekani kwa mwaka jana, na kuifanya China kuongoza katika soko hilo duniani.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na wizara ya biashara ya China, biashara hiyo iliendelea kuongezeka kwa kasi kwa asilimia 32.5 kuanzia Januari hadi Mei mwaka huu ikilinganishwa na mwaka jana wakati kama huo.
Wakati huohuo China inaendelea kutunga sheria kuhusu biashara ya mtandao wa Internet ili kuondoa matatizo yaliyopo sasa kama vile utapeli, bidhaa feki na kutumiwa vibaya kwa taarifa binafsi za wateja.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...