Arsenal ilipata ushindi mzuri dhidi ya
West Ham jana kwenye uwanja wa
Emirates, London huku ikijiandaa kwa mchuano mkali kati yake na klabu ya
Monaco siku ya jumanne.
Klabu hiyo iliyopo chini ya Arsene Wenger iliishinda West Ham kwa jumla ya mabao 3-0 na kuimarisha ndoto yake katika nafasi nne bora kwenye msimamo wa ligi ya Uingereza.
The Gunners ilitawala mechi hiyo huku Olivier Giroud akifunga bao la kwanzadk45 kabla ya kipindi cha kwanza kukamilika.

Mabao ya dakika za mwisho ya
Aaron Ramsey dk 81 na
Mathiew Flamini dk 84 yaliifanya Arsenal kufikisha pointi 57 zikiwa ni pointi nne mbele ya mabingwa wa zamani
Manchester United walio katika nafasi ya nne.

Arsenal sasa inajianda dhidi ya Monaco ya nchini Ufaransa siku ya jummane katika mechi ya ligi ya klabu bingwa barani Ulaya.
0 comments:
Post a Comment