Friday, June 17, 2016

Amchoma kwa tindi kali baada ya kukataa kumuoa Pakistan

Mwanamme mmoja wa umri wa makamu, anatibiwa katika hospitali moja nchini Pakistan baada ya kuchomwa kwa tindi kali iliyomsababishia majeraha ya asilimia hamsini.

Mwanamke anayelaumiwa kummwagia tindi kali hiyo amekamatwa.

Familia ya mwanamme huyo, inasema mwanamke alikasirika baada ya mwanamme huyo kukataa kumuoa licha ya wao kuwa na uhusiano.

Mashambulizi ya kutumia tindi kali ni mengi dhidi ya wanawake nchini Pakistan lakini sio rahisi kuendeshwa dhidi ya wanaume.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...