Wapiganaji wa dola ya Kiislam IS wamesambaza picha za video katika
mitandao kwa lengo la kuonyesha kuchinjwa kwa mwandishi wa habari raia
Marekani Steven Sotloff ambaye ni mmoja wa mateka wanaoshikiliwa na
wapiganaji hao.
Mwandishi huyo Sotloff, mwenye umri wa miaka 31 ambaye alitekwa na wapiganaji hao mwezi August mwaka jana.
Mwezi uliopita Sotloff alionekana mwishoni katika picha za video
zilizoonyeshwa kuhusiana na kuchinjwa kwa mwandishi mwingine wa Marekani
James Foley.
Baada ya mauaji ya mwandishi wa awali Foley, mama mzazi wa mwandiashi wa Sotloff alitoa ombi maalumu kwa kiongozi wa wanajeshi hao Abu Bakr al-Baghdadi kuto muua mtoto wake.
Msemaji wa Ikulu ya White House Josh Earnest amesema kuwa maofisa wa Marekani wanaendelea na uchunguzi wa ripoti hiyo.
Marekani hivi karibuni ilifanya mashambulizi ya anga dhidi ya IS nchini Iraq na inasadikika kuwa hatua hiyo ya kikundi cha IS ni visasi dhidi ya Marekani pamoja na washirika wake.
0 comments:
Post a Comment