
Hayo yanajiri katika hali ambayo, Umoja
wa Afrika (AU) umetangaza kuwa, wiki ijayo utaitisha kikao cha dharura
kwa ajili ya kukabiliana na kasi ya kuenea virusi vya homa ya Ebola
barani humo. Taarifa ya AU imesema, katika kikao hicho kutajadiliwa njia
za kuzuia kuenea virusi vya Ebola. Hadi sasa virusi vya ugonjwa huo
vimeripotiwa katika nchi za Liberia, Sierra Leone, Guinea, Nigeria,
Senegal na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambapo zaidi ya watu 1,500
wamepoteza maisha yao kutokana na maradhi hayo.
0 comments:
Post a Comment