Thursday, September 11, 2014

Video: Hakuna kuongeza sifuri: H Baba aeleza jinsi alivyotumia 150,000 tu kukamilisha video yake 'Tubabane'

Video: Hakuna kuongeza sifuri:  H Baba aeleza jinsi alivyotumia 150,000 tu kukamilisha video yake
Msanii wa miondoko ya Bongo Bolingo Flava, H Baba anaweza kuwa msanii wa kwanza mkubwa Tanzania kujitokeza hadharani kutaja kiwango kidogo zaidi alichotumia kushuti video ya wimbo wake.
Bila kung’ata neno wala kuongeza sifuri, H Baba  alieleza kuwa video ya wimbo wake mpya Tubebane aliofanya na muongozaji kutoka Mwanza ‘Saimaco’ ilimgarimu kiasi cha fedha za Kitanzania 150,000 tu.
“Unajua watu wengi wanaweza kukwambia ‘H Baba hatumuoni…’ waangalie video yangu niliyoshuti kwa 150,000 tu. Haina sifuri mbele. Ni laki na nusu na video inaitwa Tubebane. Ni bonge la video…”Alisema H Baba.
“Unajua sisi wasanii tusipende kuongea uongo kwa sababu uongo unaweza kutuletea matatizo. Matatizo ni yapi, mashabiki wanajua sisi tuna pesa kumbe pesa hatuna.” Aliongeza.Ameeleza kuwa bei hiyo imetokana na ofa aliyopewa na Saimaco kushuti video hiyo bure kabisa na gharama alizoingia ni kulipia chakula kwa watu waliohusika kukamilisha zoezi hilo na mafuta ya gari.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...