Saturday, November 23, 2013

jua afrika tulivyo pata shavu ulaya

Ban Ki-moon: Nchi za Afrika ziongeze nafasi za kazi Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesisitiza juu ya umuhimu wa kuongezwa nafasi za kazi kwa ajili ya kupunguza kiwango cha umasikini barani Afrika. Ki-moonameyasema hayo kupitia ripoti iliyosambazwa hapo jana na kusisitiza kuwa, kuongezwa nafasi za kazi ni moja ya njia muhimu za kupunguza umasikini barani humo. Katika ripoti hiyo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amefafanua kuwa, barani Afrika kuna nchi kadhaa zenye kiwango cha juu cha uchumi huku jamii nyingi ya nchi hizo ikiwa inakabiliwa na hali mbaya ya kiuchumi na kijamii, suala linalotokana na kusahauliwa na serikali zao. Ameongeza kuwa, asilimia kubwa ya vijana hawana ajira suala ambalo linatia wasiwasi mkubwa. Akizungumzia mpango wa maendeleo wa baada ya mwaka 2015 kwa ajili ya kufikiwa malengo ya milenia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa, kuna haja kwa nchi za Afrika kutatua tatizo la ukosefu wa ajira hususan kwa vijana, sanjari na kutokomeza udhoofu na badala yake kuweka miundombinu imara ya kiuchumi katika nchi hizo.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...