Kundi moja lililojihami nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati limewaingiza
karibu watoto 6000 kwa jeshi lao kwa mujibu wa shirika la kuhudumia
watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF.
Karibu nusu ya watoto hao wameingizwa jeshini mwaka huu kufuatia
kupinduliwa kwa serikali na waasi mwezi nMachi. UNICEF inasema kuwa hali
ya usalama kwenye Jamhuri ya Afrika ya kati inasalia kuwa mbaya huku
makundi yaliyojihami yakiendelesha dhuluma. Raia waliojipata ndani ya
mapigani wamebuni makundi yao ya kujilinda ambapo pia makabiliano kati
ya wakristo na waislamu yakishuhudiwa kila siku. Mkurugenzi wa UNICEF
nchini humo Souleymane Diabate hata hivyo anasema kuwa baada ya kuwepo
kwa hali mbaya ya usalama UNICEF inaendela na shughuli zake za utoaji wa
huduma za kibinadamu.
Umoja wa Mataifa unakadiria kuwa karibu nusu ya waakazi wote milioni
nne nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati wanahitaji huduma za kibinadamu.
0 comments:
Post a Comment