Saturday, November 23, 2013

update:masaa machache kabla ya show ya p squre wamesema haya

Kutoka katika mkutano na waandishi wa habari, P Square wamewaahidi watanzania onyesho la aina yake ambalo hawajawahi kuliona, ambapo kwa mujibu wao wenyewe, watakamua jukwaani si kwa masaa mawili tu kama ilivyokuwa imetangazwa awali, bali watatumbuiza mashabiki mpaka watosheke kabisa.
Wasanii hawa wametoa shukurani za kutosha kwa East Africa Radio, East Africa Television na wadhamini wengine kwa kufanikisha onyesho hili ambalo litakuwa ni la kwanza kabisa baada ya wakali hawa kusherekea siku yao ya kuzaliwa tarehe 18 mwezi huu.

Akiongea na waandishi wa habari, Mkuu wa vipindi wa East Africa Radio Bwana Nasser Kingu amewataka mashabiki kuwahi uwanjani katika burudani hii ambayo amesema itaanza saa moja kamili usiku, siku ya kesho tarehe 23 Novemba ndani ya viwanja vya Leaders Club.

Kwa niaba ya wasanii kutoka hapa hapa nyumbani ambao wote walikuwepo kuwakilisha katika mkutano na waandishi, Lady Jay Dee amewataka watanzania kuhakikisha hawakosi burudani hii ya aina yake.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...