Wednesday, March 19, 2014

+254:victoria kimani amepiga picha na wasanii wengi

Victoria Kimani asema amepiga picha na wasanii wengi wakubwa duniani na hakuna mengine yanayoendelea zaidi ya kazi
Mwanamuziki wa kike wa Kenya, Victoria Kimani ameamua kusema na mashabiki wake kwa lugha ya Kiswahili kupitia Instagram.
Mwimbaji huyo wa Chocolate City ambaye alishafanya kazi na wasanii wakubwa duniani kama Busta Rhymes amezungumzia sakata la kuonekana katika picha na baadhi ya wasanii wakubwa na kuhusishwa na uhusiano wa mapenzi. Suala ambalo lilizuka baada ya kupiga picha na Diamond Platinumz walipokutana Afrika Kusini.
Victoria ameeleza kuwa kupiga picha hakumaanishi kuwa kuna kitu chochote kinachoendelea zaidi ya kazi ya muziki.
Katika hatua nyingine, Victoria ameonesha furaha yake kwa kufanya kazi ya pamoja na wasani wa Tanzania wanaofanya vizuri kwenye game la Bongo Flava, Diamond na Ommy Dimpoz akiwa msanii wa kwanza wa kike kuwakutanisha wakali hao.
Huu ndio ujumbe alioandika Victoria Kimani.
“Mafans wangu wote, nawapenda sana sana. Nafanya kazi ya muziki kwa bidii na kwa sababu yenu. Nimepiga picha na wanamuziki wengi na wakubwa sana kote duniani. Na hiyo HAIMAANISHI KUNA MAMBO MENGINE YANAENDELEA NJE ya KAZI YA MUZIKI. Kwa hayo machache, ninafuraha sana kufanya kazi na wanamuziki wakubwa zaidi wa Bongo @ommydimpoz na @diamondplatnumz kwenye single moja. Mimi ndiye msanii wa kwanza wakike kufanya single moja na hawa wawili. Tunafocus na mambo makubwa zaidi ili East Africa iende mbele kimuziki. NAWAPENDA WOTE. Mimi wenu VICTORIA KIMANI .” 

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...