Thursday, July 3, 2014

Baada ya kutolewa na Ujerumani, Algeria yapata mapokezi ya kishujaa

Video: Baada ya kutolewa na Ujerumani, Algeria yapata mapokezi ya kishujaa
Waliokuwa wawakilishi wa bara la Afrika kwenye fainali za kombe la dunia zinazoendelea nchini Brazil timu ya taifa ya Algeria, wamerejea nyumbani na kupokewa kishujaa na mashabiki wa soka waliokuwa wamejitokeza kwenye uwanja wa ndege wa mjini Algiers
Algeria wamerejea nyumbani, baada ya kutolewa kwenye fainali hizo ambazo zinaingia kwenye hatua ya robo fainali, huku wakiweka rekodi ya kufika kwa mara ya kwanza kwenye hatua ya 16 bora.
Mara baada ya kuwasili nyumbani wachezaji wa timu ya taifa ya Algeria walipanda gari la wazi na kupita katika mitaa mbalimbali ya mji wa Algiers kwa ajili ya kuwasalimu mashabiki ambao walijipanga pembezoni mwa barabara kuwasubiri.
Hata hivyo mashabiki wengine walikwenda sambamba na gari hilo la wazi kwa kutembea kwa mguu ikiwa ni kuonyesha ni vipi walivyopendezwa na uwezo waliouonyesha wakati wakiwa nchini Brazil, kabla ya kutolewa na Ujerumani kwenye mchezo wa hatua ya 16 bora kwa kufungwa mabao mawili kwa moja.http://www.dailymotion.com/video/x20obvn_arrivee-de-l-equipe-nationale-a-alger-apres-le-mondial-bresilien_sportFIFA wameizawadiwa timu ya taifa ya Algeria dola za kimarekani million 9 ambazo hutolewa kwa timu zote zilizofanikiwa kutinga kwenye hatua ya 16 bora.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...