Thursday, July 3, 2014

Video: Sakata la upangaji wa matokeo, FIFA watoa ahadi yao

Video: Sakata la upangaji wa matokeo, FIFA watoa ahadi yao
Shirikisho la soka duniani FIFA limeahidi kutoa ushirikiano wa dhati kwa baadhi ya vyombo vya habari, ambavyo vinaendelea kuibua taarifa za hofu ya upangaji wa matokeo kwa baadhi ya timu ambazo zilifuzu kucheza fainali za kombe la dunia mwaka huu.
Msemaji wa shirikisho hilo Rob Harris, amesema FIFA itaonyesha ushirikiano kwa chombo chochote cha habari ambacho kitawasilisha ushahidi wa kutosha, ambao utawashurutisha kuamini ni kweli kuna jambo hilo ambalo linapigwa vita katika michezo.
Harris, amesema ni vigumu kwa sasa kutoa tamko lolote ama kuanza kufanya uchuguzi kupitia taarifa ambazo zinaandikwa katika vyombo vya habari vya nchini Uingereza pamoja na Ujerumani kwa kudai kuna harufu ya mchezo mchafu wa upangaji wa matokeo.
Katika hatua nyingine msemaji huyo wa FIFA amesema mpaka sasa hawajaona dalili zozote ambazo zinahusiana na mchezo mchafu wa upangaji wa matokeo, hivyo wamevitaka vyombo vya habarti kuwa makini na taarifa wanazozitoa kwenye jamii ya soka.

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...