Mwimbaji nyota wa muziki wa injili nchini Tanzania Rose Muhando
anatarajia kuwashirikisha waimbaji nyota wa miondoko hiyo Afrika
Mashariki katika uzinduzi wa albamu yake aliyoibatiza jina 'Kamata Pindo
la Yesu'.
Gwiji
huyo yupo katika mpango wa kuizindua albamu hiyo tarehe 3 mwezi Agosti
mwaka huu jijini Dar es Salaam ambapo amegusia kuwa bado hajaweka
hadharani orodha nzima ya waimbaji ambao watamsindikiza stejini japo
kuwa ana mpango wa kumwalika mwanadada Anastazia Mukabwa kutoka nchini
Kenya aliyeshirki katika wimbo wake Rose uitwao 'Kiatu Kivue'.
Rose Muhando ameelezea kuwa albamu yake hiyo mpya imesheheni nyimbo zikiwemo Bwana Niongoze, Wewe Waweza, Usiniache, Kamata Pindo la Yesu, Facebook na nyinginezo nyingi.
Rose Muhando ameelezea kuwa albamu yake hiyo mpya imesheheni nyimbo zikiwemo Bwana Niongoze, Wewe Waweza, Usiniache, Kamata Pindo la Yesu, Facebook na nyinginezo nyingi.

0 comments:
Post a Comment