Sunday, August 31, 2014

Ukarabati kituo cha umeme Kipawa karibu kukamilika

Kazi ya ukarabati wa kituo kikubwa cha kusambazia umeme cha Kipawa ambacho kilipata hitilafu na kuharibika juzi saa Saba usiku inaelekea kukamilika baada ya maeneo mengi yaliyoathiriwa na hitilafu hiyo kuanza kupata umeme.
Meneja wa Tanesco mkoa wa Ilala mhandisi Atanasius Nangali, ameiambia East Africa Radio kuwa kazi ya ukarabati inaendelea vizuri ambapo mafundi wa shirika hilo wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana kuhakikisha umeme unarejea.
Ameyataja maeneo ambayo bado umeme haujarejea mpaka sasa kuwa ni Gongolamboto, Kivule na Kipunguni na kwamba muda wowote kuanzia sasa umeme katika maeneo hayo utarudi katika hali yake ya kawaida.
Kwa mujibu wa mhandisi Nangali, hitilafu hiyo ilisababisha maeneo mengi ya wilaya za Temeke, Ilala na Kisarawe kukosa nishati ya umeme, na kwamba juhudi zilifanyika za kurejesha umeme katika maeneo nyeti ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere ambako mafundi wa TANESCO mkoa wa Ilala waliandaa njia ya moja kwa moja ya umeme kutoka maeneo mengine ya jiji kuelekea uwanjani hapo.
Aidha, mhandisi Nangali amesema hitilafu hiyo ni ya kiufundi na kuongeza kuwa matukio ya aina hiyo yamekuwa nadra hivi sasa kwani shirika limeimarisha ukarabati wa miundombinu yake ikiwa ni pamoja na njia zilizochakaa pamoja na mifumo ya usambazaji.

Video: Matokeo Ya Sare dhidi ya Leicester City Yasababisha Wenger Kuitwa Dikteta

Video: Matokeo Ya Sare dhidi ya Leicester City Yasababisha Wenger Kuitwa Dikteta
Baada ya kulazimishwa matokeo ya sare ya bao moja kwa moja dhidi ya Leicester City, mashabiki wa klabu ya Arsenal wamembwatukia meneja wa kikosi chao Arsene Wenger na kumuita dikteta.
Wakizungumza kwa hasira mara baada ya mchezo huo ambao uliunguruma mjini Leicester katika uwanja wa King Power mashabiki hao wamesema, Arsene wenger amekuwa na sababu za makusudi kuiona klabu yao inafanya vibaya huku akitambua fika kinachosumbua kikosini.
Wasema yeye kama meneja siku zote amekua anahisi ndie mtu pekee anaijua sana Arsenal na wala hafikirii kama kuna watu wengine wanaumizwa na kinachotokea uwanjani.
Mmoja wa mashabiki hao amesema ilimuumiza sana kuona mchezo na matokeo yaliyopatikana na ilifikia hatua alijilaumu kwa nini alisafiri kutoka jijini London kuelekea mjini Leicester kwa ajili ya kuishangilia timu yake.
Amesema endapo mzee huyo kutoka nchini Ufaransa atashindwa kubadilika kuna hatari kubwa ya kuendelea kufanya vibaya na mwisho wa yote watashindwa kupambana na timu kubwa kama Chelsea, Man City, Liverpool pamoja na Man utd.
Shabiki mwingine alionyesha hisia zake kwa kusema haiwezekani kila msimu mtu mmoja kuwaumiza kwa kushindwa kufanya maamuzi ya kuwasajili wachezaji ambao wataweza kuleta changamoto mpya na mwishowe wafikie mafanikio kama ilivyo kwa klabu nyingine.
Amesema Arsene Wenger hastahili kufanya kazi kubwa zaidi ya kufanya usajili wa mchezaji anaecheza nafasi ya ushambuliaji pamoja na kiungo mkabaji.
Kwa matokeo ya jana ya sare ya bao moja kwa moja yanaiacha Arsenal ikiwa na point tano huku ikitarajia kupambana na Man City katika mchezo ujao mnamo Septemba 13.

Alichoamua Britney Spears baada ya kuona video ya mpenzi wake akimsaliti

Alichoamua Britney Spears baada ya kuona video ya mpenzi wake akimsaliti
Mwimbaji Britney Spears amevunjwa moyo baada ya kushuhudia kipande cha video kilichovujishwa kikimuonesha mpenzi wake David Lucado akimsaliti na msichana ambaye hakutambulika kwa haraka.
Katika video hiyo, David Lucado anaonekana akicheza na msichana huyo huku akimkiss kama wanaigiza filamu ya mahaba na wao ndio wahusika wakuu.
Britney Spears ameshindwa kuvumilia alichokiona na ameamua kumpiga chini Lucado na hivi ni single girl.
“Aahhhh! The Single life.” Ametweet Britney.

Unyanyasaji Mtandano + Kifo cha Betty Ndejembi, nani wa kumnyooshea kidole?


Imeandikwa na Malisa Godlisten
Ninaandika makala hii nikitambua bayana kuwa itamuudhi kila mtu anayeingia mtandaoni kwa minajili ya kuwanyanyasa wengine. Lakini siku zote ninaamini katika busara hii: kuuchukia ukweli hakubadilishi ukweli kuwa uongo. Ukweli ni ukweli na uongo ni uongo. Ukweli hauwezi kuwa uongo, na kadhalika uongo hauwezi kuwa ukweli. Kamwe asilani. Wakati tunaomboleza kifo cha ndugu yetu Betty Ndejembi watu wamesema mengi, na yameandikwa mengi. Kila mmoja kwa namna alivyoguswa. Zitto kabwe ametweet hivi asubuhi “justice for bett”, akitoa rai haki ipatikane kwenye kifo cha Betty.Unyanyasaji Mtandano + Kifo cha Betty Ndejembi, nani wa kumnyooshea kidole?
Marehemu Betty Ndejembi
Jokate Mwegelo naye ametweet kuomba msaada wa kuchunguza kifo cha Betty. Na watu wengine maarufu kila mmoja kasema neno, labda kwa sababu Betty alikuwa maarufu in one way or another. Lakini hatuwezi kukwepa ukweli kwamba siku chache kabla ya kifo chake, alinyanyaswa mno kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter.
Japo hadi muda huu hatuwezi kuhusisha moja kwa moja uhusiano kati ya unyanyasaji huo na kifo chake, lakini mtu akinyanyaswa masaa kadhaa kabla ya kifo chake, waweza kujenga picha fulani. Saa chache kabla ya kifo chake Betty alitweet, “ITS ALWAYS THE PEOPLE YOU TRUST WILL DO THEOST DAMAGE TO YOU...ITS BEEN A GOOD LIFE THO”
Baada ya kutweet hakuonekana tena hadi alipookotwa mtaroni kesho yake asubuhi akiwa amefanyia vitendo vya kikatili na akiwa amepoteza fahamu.
Lakini kabla hata ya kutweet hivyo, Betty alikuwa anaandamwa sana mtandaoni huko Twitter. Kuna watu walianzisha team ya kumtukana, kumjibu hovyo na kumprovoke kwa kila alilofanya. Naomba ieleweke kuwa simlaumu mtu kwa sababu sina mamlaka ya kufanya hivyo bali dhima ya makala hii ni rambirambi zangu kwa Betty kuzungumzia tatizo la unyanyasaji mtandaoni, sambamba na suala zima la unafiki kila kinapojiri kifo hususani cha mtu maarufu. Tuna tatizo kubwa huko mitandaoni.
Tumefika hatua ya kuwapa umaarufu watu wenye matusi ya nguoni, wazushi, wambeya, wanafiki. Wanaochafua wenzao, kutishia wenzao kwa kujifanya askari jkt, kusengenya na kupost majungu…. Aina ya binaadamu wanaostahili laana lakini twaishia kuwatukuza
Kwenye hii mitandao, matusi imekuwa njia ya mkato ya kupata umaarufu. Kuna wenzetu wengi tu wenye ‘umaarufu’ huko twitter, facebook na instagram lakini ukidadisi chanzo cha ‘umaarufu’ huo, utaambiwa ‘ah huyu ana matusi si mchezo’. Kuna watu wazima na akili zao wanatumia muda mwingi kwenye mitandao ya kijamii aidha kunyanyasa wenzao kama si kusherehesha unyanyasaji huo. Marehemu Betty ni victim wa yote hayo.
Alitukanwa sana, na aliitwa majina kadhaa ya kumdhihaki kabla ya kukutana na mauti.
Kuna waliomwita Di maria, superstar uchwara etc.. and I hope hao waliomuita hivyo wanajifahamu na wengine wananisoma hapa. Japo sijui chanzo cha ‘ugomvi’ wao, lakini naamini kuna watu wengi tu waliokuwa katika nafasi ya kuzima moto huo kwa vile walikuwa wakizifahamu pande zote mbili za ‘ugomvi’ husika lakini kwa sababu ya unafiki wakapalilia moto maana wanafurahi watu wakigombana.
La kukera zaidi ambalo ni wazi litajichomoza wakati wa maombolezo haya ni unafiki. Watu walewale waliodiriki kumwandama marehemu wakati wa uhai wake watageuka kuwa wenye uchungu mkubwa baada ya kifo chake.
Hii inanikumbusha suala ambalo nimeshawahi kulizungumzia mara kadhaa kwamba ‘wakati’ muafaka wa kutafuta vipaji vya uigizaji ni kwenye misiba: watu walewale waliokuwa wakikuchukia kwa nguvu zote watageuka wenye uchungu mkubwa kwa kifo chako.’ Ukiangalia baadhi ya tweets za mwisho za marehemu ni wazi kuwa binti huyo alikuwa anahitaji msaada kutoka kwa wanaomjali. Mojawapo ya tweet za mwishomwisho za marehemu alisema hivi.
‘Thank you all for the names  I was called, luck y’all have such a perfect life.! No hard feelings.. I’m alive still.! Endeleeni kuongea.’
 Kwa tafsiri isiyo rasmi Betty alisema, ‘asanteni kwa majina yote mliyoniita. Mmebarikiwa kuwa na maisha mazuri.! Hamuumizwi na hisia kama mimi. Ila bado ninaishi, endeleeni kuongea.’
Kwa bahati mbaya hakuna aliyejali, hadi juzi asubuhi (Jumatano) Betty alipookotwa kwenye mtaro akiwa amefanyiwa unyanyasaji wa kijinsia na akiwa amepoteza fahamu. Kifo cha Betty ni miongoni mwa vifo vya kikatili sana kuwahi kutokea nchini. Nashauri wanaharakati ea haki za wanawake wapambane kuhakikisha haki inapatikana.
Akina Annanilea Nkya, Hellen Kijobisimba watafute haki ya binti huyu kama Zitto Kabwe alivyosema ‘justice for betty’, imagine mtu aliyekua kwenye maumivu makali ya hisia, anatekwa na genge la wahuni. Bila kujali kipindi kigumu alichokua anapitia, bila kujali hakua na wazazi, bila kujali psychological torture aliyokua nayo still wanamfanyia unyanyasaji wa kijinsia hadi anapoteza fahamu.
Betty aliokotwa mtaroni na kupelekwa hospitali. Jana (Alhamisi) aliweza kufungua macho, lakini hakuweza kuongea lolote hadi saa 3 usiku wa kuamkia leo, mauti ilipomkuta. Kwaheri betty, kwaheri classmate wangu (Majengo sec). Kwaheri rafiki, kwaheri ndugu. Umeondoka dunia bado inakuhitaji. Naumia you have gone too young, lakini naumia zaidi sababu umekufa kikatili mno.
Japo sijui nitakufaje, lakini nadiriki kusema hukustahili kifo cha aina hii. Nakumbuka sms yako ya mwisho kwangu uliniambia hivi, ‘Malisa blv me, only youths can change this country.’ Leo nilipopata taarifa ya kifo chako nimerudia kuisoma sms yako mara mbilimbili.
Sikujua kuwa sms hiyo ndo ulikua unaniaga. Umeniaga kwa kutuachia vijana wosia, kuwa vijana pekee ndio wenye uwezo wa kuibadilisha nchi hii. Nitakua nimekusaliti ikiwa sitautendea kazi wosia huu. I promise to fight and motivate other youths to liberate this country for your dedication. Umekwenda kumfuata mama yako, umemfuata baba yako. Wazazi wako walitangulia, leo wewe umewafuata. Hatimaye familia nzima mmekutana Paradiso.
Huu ni baadhi ya ujumbe uliondikwa na watu mbalimbali waliokuwa wakimfahamu Betty:
Faraja Nyalandu:
Kifo cha Betty kimetuachia mafundisho mengi. Natumai kila mmoja aliyemfahamu Betty kwa namna moja ama nyingine amepata lake la kujifunza. Gharama ya mafundisho tuliyoyapata ni kubwa sana. Maumivu. Kifo. Aliyelipa ni Betty na wanaompenda. Itafaa gharama hii isiende bure. Tuwe wakarimu. Tuwe na upendo. Tumshike mtu mkono pale alipo na uhitaji. Tumnyanyue akianguka. Lakini vyote haviwezi kuwa kama ndani yetu havipo. Huwezi kutoa ambacho huna. Tuanze ndani yetu. Betty tusamehe. Mungu atusamehe na Mungu atusaidie. Pumzika kwa amani Betty.

Ukatili na unyanyasaji wa aina yoyote ni kinyume cha haki za binadamu, tupaze sauti kwa pamoja na kuchukua hatua. Vitendo hivi havikubaliki.
‘Justice for Betty’..Apumzike kwa Amani.

Ujerumani si shwari tena

POLISI UJERUMANI WAMUOKOA DIAMOND KUTOKA KWA WASHABIKI WENYE HASIRA ! KASHINDWA KUWIKA STUTTGART KISA ?

KAFIKA UKUMBINI SAA 10 ALFAJIRI ! WASHABIKI WANASURI SHOW TANGU SAA 4 USIKU

PROMOTA MNAIJERIA AINGIA MITINI ,DJ APATA KISAGO HETI VYOMBO VIBOVU ! HAIBU

Stuttgart,Ujerumani,
Usiku wa Jumamosi ya Tarehe  30.Augost 2014, majira ya saa 10 alfajiri
Mwanamuziki nyota wa Bongo Flaver  Nasib Abdul aka Diamond Platnumz alijukuta katika hali ya hatari hadi kuokolewa na Polisi mjini Stuttgart,ujerumani,baada ya washabiki waliokuwa na hasira kuchoka kusubiri show,washabiki hao waliokuwa wamelipa ticket euro 25 kwa kiingilio walihadiwa kuwa show ingeanza saa 4.00 usiku,lakini walijukuta wakisubiri hadi majira ya saa10 usiku au alfajiri ndipo mwanamuziki Diamond alipoletwa jukwaani na promota wake raia wa Nigeria anajiita kama Britts Event.
Hapo ndipo washabiki walipoona kuwa hawakutendewa haki walianza kurusha chupa na kutaka kumvamia mwanamuziki  Diamond na promota wake,
Kilichowakera zaidi washabiki ni pamoja na vyombo vibovu vilivyofungwa katika ukumbi huo kitu ambacho kiliwafanya washabiki kuvunja hadi vyombo vya muziki
ma-Djs walishambuliwa na wapo Hosptalini kwa sasa.moja wa Djs hao alipoteza Lap top yake ,mwanadada DJ  Flor alipatwa shock mstuko wa moyo na kukimbizwa hosptali, washabiki hao walimpa kipigo  DJ Drazee naye yupo hoi hospatal. Polisi nchini ujerumani wanamesema tukio hili la haibu alijawahi kutokea,kuwa msanii kuchelewa kufika jukwaani kwa ujerumani ni kitu cha hatari kwani washabiki wa ujerumani wanaheshimu sana muda wao.
mpaka sasa polisi wanamsaka mwandaaji wa onyesho hilo na wamesema kuwa
wanachunguza thamani ya hasara hiliyosababishwa na ghasia hizo na pia itamfungulia mashataka promoter huyo raia wa Nigeria,ambaye pia anachunguzwa kwa kusemekana anajihusisha na mtandao fulani wa biashara.

Magazeti ya Stuttgart; yameandika "Washabiki wa hasira nawe DIAMOND"  link:

mr.nay yajaa soon

Video ya msanii Ney Wa Mitego, Mr Nay ambayo picha za utayarishaji wake ziliwatisha kidogo mashabiki kutokana na kuhusisha matukio yenye ishara zinazohusishwa na imani za kishetani, imetoka rasmi kwa ajili ya mashabiki wa msanii huyu.
Video hii ya Mr Nay imefanyika huko nchini Kenya chini ya muongozaji Kevin Bosco Junior, kazi ambayo audio yake imefanyika chini ya mtayarishaji mahiri anayefanya kazi na msanii huyu, Mr T Touchez.

mabaga fresh wanakuja tena


Lile kundi lililotamba miaka ya nyuma katika muziki wa Bongo Flava ambalo liliwahusisha walemavu wenye vipaji wawili na kujipa jina Mabaga Fresh, limeamua kuungana tena katika gemu kwa kuachia wimbo wao mpya.
 DJ Snox amesema baada ya kutengena kwa muda mrefu na mwenzake kujiunga na TMK Wanaume Halisi na yeye kufanya kazi binafsi, wameonesha nia ya mashabiki wao kuwaona tena pamoja ndio wameamua kuanza kufanya kazi pamoja.
Kundi hilo linaundwa na watu wawili ambao ni Dj Snox n JB mkubwa wa Majaji ambao walitamba na nyimbo kama Mtulize, Tunataabika, Hakuna Noma na nyingine kibao.
Sasa mashabiki wa TMK na Mabaga Fresh ndio ujio mpya tena na wimbo wao wa USIMPE POMBE.

picha:kim kardashian anaonekana hivi kwa sasa

kim (3)kim (7)kimkim (9)kim (6)kim (2)kim (5)

Baada ya kuondoka kwa Torres – huyu ndio mshambuliaji mpya aliyesajiliwa na Chelsea

IMG_6889.JPGUsiku wa jana mshambuliaji wa kimataifa wa Spain Fernando Torres alikamilisha usajili wake wa mkopo wa miaka miwili kutoka Chelsea kwenda AC Milan.
Huku yakiwa hajapita hata masaa 24 tangu Torres aondoke, Jose Mourinho amekamilisha usajili wa mbadala wa Torres, mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Loic Remy.
Remy ambaye alifeli vipimo vya afya alipokuwa akikaribia kujiunga na Liverpool mwanzoni mwa dirisha la usajili, amejiunga na Chelsea kwa ada ya uhamisho wa paundi millioni 10 kutoka QPR.
Remy anachukua nafasi ya Torres na kuungana na Didier Drogba katika kumsaidia Diego Costa.
Wakati huo huo Alex Song amejiunga na West Ham kwa mkopo kutoka FC Barcelona.IMG_6888.JPG

Gelly asema muziki umebadilika, na yeye abadilika

Staa wa muziki Gelly wa Rhymes, ameweka wazi kuwa kwa sasa katika soko la muziki, yeye akiwa kama msanii mwenye muda katika game ameona mabadiliko makubwa na vipaji vipya vinavyofanya vizuri.
Gelly amesema kuwa kwa sasa muziki Bongo umeenda kimataifa zaidi kulenga soko la Afrika, na hii ndiyo sababu ya ngoma yake mpya aliyoachia wiki hii, Iyolele, kusukwa kwa lengo la kutosheleza soko hili.
Gelly wa Rhymes amesema kuwa, kwa sasa amekuja na mkakati ya kuliteka soko la Afrika kupitia muziki wake na pia video ya kazi zake ambazo kwa upande wake amejikita kuzitengenezea hapa hapa nchini kwa imani kuwa inawezekana kutengeneza kazi ya kiwango cha juu hapa hapa nyumbani endapo mtu atajipanga.

Stereo: ilinibidi kuisubiri Usione Hatari

Rapa Stereo ambaye ameachia kwa mashabiki wake kolabo yake ya Kimataifa, "Wako", featuring Victoria Kimani, ameweka wazi sababu za kazi hii kuchelewa kuachiwa, ambapo amesema kuwa ni kutokana na Video ya Usione Hatari kuchelewa kutoka.
Stereo amesema kuwa, aliamua kutoa muda kwa kazi yake hii iliyotangulia, Usione Hatari kuwakaa mashabiki wake kabla ya kuwahamishia katika jiwe jingine, Wako ambalo tayari limepokelewa vizuri mitaani na mashabiki wa muziki.
Kuhusiana na video ya kazi hii mpya ya kimataifa, Stereo amesema kuwa baada ya wiki mbili tatu, atakuwa ameweka mambo kwenye mstari.

Video Mpya: Ejeajo- P Square Feat. T.I

Video Mpya: Ejeajo- P Square Feat. T.I
P Square wamempa shavu rapper T.I kwenye wimbo wao mpya ‘Ejeajo’ uliotoka na video yenye move kali za Michael Jackson.
Iangalie hapa:

Mapya kuhusu mtoto wa Jackie Chan aliyekamatwa na dawa za kulevya

Mapya kuhusu mtoto wa Jackie Chan aliyekamatwa na dawa za kulevyaMtoto wa Jackie Chan ambaye pia ni muigizaji wa filamu za mapigano, Jaycee Chan anaendelea kushikiliwa na polisi nchini China kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya.
Kwa mujibu wa polisi wa Beijing, Jaycee alikamatwa akiwa na muigizaji mwenzake wa Taiwan, Kai Ko na kwamba baada ya kupimwa waligundulika kuwa walikuwa wametumia dawa za kulevya aina ya marijuana.
Jaycee na Kai Ko wamekiri kutumia dawa hizo na kueleza kuwa grams 100 za dawa hizo zilipelekwa nyumbani kwa Jaycee (mtoto wa Jackie Chan).
Baada ya kushikiliwa kwa wiki mbili (tangu August 14), Kai Ko ameachiwa Ijumaa iliyopita na anasubiri taratibu zaidi za kisheria huku Jaycee akiendelea kusota rumande.
Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Beijing, waandishi wa habari walimfuata Kai Ko hadi kwenye hotel aliyofikia lakini hakuonesha ushirikiano na alijaribu kumpiga mwandishi mmoja kabla hajaingia kwenye lift na kutokomea.
Baada ya kukamatwa na dawa hizo, Jackie Chan aliomba radhi umma kwa niaba ya mwanae na familia yao kwa ujumla alimtaka mwanae kuelewa kuwa amefanya makosa na anapaswa kukutana na matokeo yake.

Thursday, August 28, 2014

Miley Cyrus amtetea kijana wake wa Mtaani anaesakwa na polisi

 Miley Cyrus amtetea kijana wake wa Mtaani anaesakwa na polisi
Baada ya kuripotiwa habari kuwa kijana wa mtaani, Jesse Helt aliyepanda jukwaani na Miley Cyrus wakati wa utoaji tuzo za MTV VMAs anasakwa na polisi kwa kosa la kuvunja masharti ya probation, Miley Cyrus amemtetea kupitia akaunti yake ya Twitter.
Miley amevilaumu vyombo vya habari kwa kujikita katika habari ya yeye kusakwa na polisi badala ya kuripoti zaidi kuhusu tatizo la vijana  wasio na makazi alilolizungumzia katika jukwaa hilo.
Jesse Helt alipanda jukwaani na Miley Cyrus na kupokea tuzo ya video bora ya mwaka kwa niaba yake na kisha kutoa hotuba fupi kuhamasisha watu kuliangalia tatizo la vijana wanaoishi katika mazingira magumu (wasio na makazi).

Wednesday, August 27, 2014

Kanye West afichua kuwa baba yake pia alikuwa Paparazzi, aeleza sababu za kumpiga paparazzi

Kanye West afichua kuwa baba yake pia alikuwa Paparazzi, aeleza sababu za kumpiga paparazzi
Kanye West ambaye mwaka jana alikuwa na ugomvi mkubwa na wapiga picha (Paparazzi) na kufikia hatua ya kumshambulia Paparazzi Daniel Ramos katika uwanja wa ndege Los Angeles amefichua kuwa baba yake mzazi aliwahi kuwa paparazzi pia.
Kwa mujibu wa MailOnline ambao wamepata nakala ya discussion  ya maridhiano kati ya Kanye West na mwanasheria wa paparazzi Ramos aitwae Nate Goldberg, rapper huyo alitoa siri hiyo wakati wa maongezi.
Kanye alieleza kuwa wazazi wake hawakumlea kuja kupigana mieleka hadharani na wapiga picha.
“My father was a paparazzo himself. My father was a medical illustrator, a Black Panther, a Christian marriage counsellor. My mother was the first black chair of the English department in Chicago State. They didn't raise me to be out here wrestling with random paparazzi in front of LAX."
Rapper huyo alisikika akieleza kuwa mara nyingi amekuwa akipata msaada kutoka kwa Paparazzi ambao wamekuwa wakimsaidia kuegesha gari lake, kulilinda wakati hayupo na hata kuhakikisha hasumbuliwi na polisi baada ya kuegesha gari lake.
“Kuna watu wema huko nje wanaojaribu kuzilisha familia zao (kupitia upigaji picha) na pia kuna wapumbavu kama huyu jamaa unaemuwakilisha.” Kanye West alimwambia mwanasheria huyo.

Polisi Arusha yamkamata 'mdunguaji risasi wanawake

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amesema jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa wa matukio ya kuwapiga risasi wanawake jijini Arusha.
Mtu huyo ni Adam Mussa, mwenye umuri wa miaka 30, mkazi wa Majengo Jijini Arusha ambaye amekamatwa na bastola mbili zikiwa na risasi kumi.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo , Kamanda Liberatus Sabas amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti 26 mwaka huu, majira ya usiku, nyumbani kwake Majengo Juu.
Kamanda Sabas amesema baada ya kumkamata mtuhumiwa na kumhoji ambapo alikiri kuhusika katika matukio yanayoendelea jijini Arusha ya upigaji wanawake risasi na moja kati ya silaha hizo iliibiwa ndani ya gari la mfanyabiashara Seleman Bakari Msuya mkazi wa Sombetini, baada ya watu wasiojulikana kuvunja kioo cha gari na kuichukua. Mtuhumiwa anatarakiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kumalizika.
Kamanda Sabas ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa siri za mtandao huo uliozuka ghafla mwezo Agosti mwaka huu na kujeruhi na kuua wanawake wenye magari mjini Arusha, ambapo hadi sasa tayari watu nane wanashikiliwa kwa kuhusiana na matukio hayo.

Magesa Mulongo ataka utulivu jijini Arusha

Mkuu wa mkoa wa Arusha Magesa Mulongo amesema kamati ya ulinzi na usalama haip tayari kuona watu wake wanapoteza maisha na kuwataka wakazi wa Arusha hususani wanawake kuwa watulivu kwa kuwa mamlaka zinalifanyia kazi suala la mauaji ya wanawake.
Wito wa mkuu wa mkoa umekuja huku kukiwa na taarifa za wanawake kukutana leo katika ofisi za mkuu wa mkoa wa Arusha kupinga mauwaji ambayo mpaka sasa jeshi la polisi limedhibitisha watu watu wawili kuuwawa na mwingine mmoja kujeruhiwa.
Akiongea na waandishi wa habari jana kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amesema idadi ya watuhumiwa kuhusiana na matukio hayo ya upigaji risasi wanawake jijini Arusha imefika nane baada ya jana mtuhumiwa Adamu Juma ambae tayari amekiri kushiriki katika matukio kadhaa kukamatwa.
Kauli ya mkuu wa mkoa Mulongo imekuja siku moja baada ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas kusema kuwa jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa Adam Mussa mwenye umuri wa miaka 30, mkazi wa Majengo Jijini Arusha, kwa kukamatwa na bastola mbili zikiwa na risasi, ambaye anatuhimwa kuhusika na matukio ya kuwapiga risasi wanawake mjini Arusha.
Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake leo , Kamanda Liberatus Sabas amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti 26 mwaka huu, majira ya usiku, nyumbani kwake Majengo Juu.
Kamanda Sabas amesema baada ya kumkamata mtuhumiwa na kumhoji ambapo alikiri kuhusika katika matukio yanayoendelea jijini Arusha ya upigaji wanawake risasi na moja kati ya silaha hizo iliibiwa ndani ya gari la mfanyabiashara Seleman Bakari Msuya mkazi wa Sombetini, baada ya watu wasiojulikana kuvunja kioo cha gari na kuichukua. Mtuhumiwa anatarakiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kumalizika.
Kamanda Sabas ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa siri za mtandao huo uliozuka ghafla mwezo Agosti mwaka huu na kujeruhi na kuua
wanawake wenye magari mjini Arusha, ambapo hadi sasa tayari watu nane wanashikiliwa kwa kuhusiana na matukio hayo.

Waombaji ajira wazingatie taratibu - serikali

Serikali ya Tanzania imewataka waombaji wa kazi kuzingatia taratibu zinazotakiwa katika kuwasilisha maombi ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza kutokana na kuwepo wa tatizo la kuwasilisha nyaraka pungufu
.
Waziri wa Kazi na Ajira nchini Tanzania, Bi. Gaudensia Kabaka.
Akizungumza Jijini Dar es Salaam Msemaji wa Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, Riziki Abraham amesema kumekuwepo na kutokufuata taratibu kwa waombaji wa kazi kutoka na baadhi yao kuwa na nyaraka ambazo hazikidhi vigezo vinavyotakiwa kwa mujibu wa tangazo la kazi.
Hata hivyo Bi. Riziki amewataka wote ambao wamepotelewa, kuharibikiwa na vyeti vya kitaaluma wanatakiwa kupeleka taarifa za kupotelewa katika mamlaka husika ili waweze kupewa taratibu za kupata vyeti vingine.
Wakati huo huo, Mamlaka ya mafunzo ya ufundi stadi Nchini (Veta) Nyanda za Juu Kusini, imefunga vyuo saba vya binafsi vya mafunzo ya hoteli na utalii Nyanda za Juu Kusini kutokana na kukiuka taratibu kwa kuendesha mafunzo bila kusajiliwa.
Mratibu wa Veta Nyanda za Juu Kusini, John Mwanja, amesema kuwa wamefikia hatua ya kuvifunga vyuo hivyo kutokana na kukosa sifa za kutoa mafunzo kutokana na kutokidhi vigezo ikiwemo usajili na vifaa vya kujifunzia.
Miongoni mwa vyuo vilivyofungwa ni Msoma Utalii tawi la Njombe, Eckross Tourism Collage,Chuo Cha Utalii Mosemi na Hokaido VTC kwa mkoa wa Njombe,na Capricon Collage, Iringa Hotel and Tourism Collage na Mufindi Tourism Collage vyote vya Mkoa wa Iringa.
Baadhi ya wanafunzi wa vyuo hivyo walilalamikia hatua ya wamiliki wa vyuo hivyo kwa kuwadanganya kuwa vyuo hivyo vimesajiliwa ilihali havijasajiliwa na hivyo kuwaibia wananchi na kuiomba serikali kuchukua hatua kali kwa wahusika.
Katika hatua nyingine, nchi wanachama wa jumuiya ya maendeleo SADC zimetakiwa kuondolewa kanuni na vikwazo vinavyokwamisha biashara na kurudisha nyuma jitihada za wanachama kujikwamua kiuchumi.
Akizungumza jijini Dar es salaam Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Biashara kutoka wizara ya viwanda na biashara Ismail Mfinanga katika mkutano wa wanachama wa jumuiya hiyo amesema vikwazo katika baishara ndani ya nchi wanachama vimekua vikitokea kutokana na mawasiliano duni.
Mfinanga ameongeza kuwa kuondolewa kwa vikwazo hivyo kutaweza kukuza masoko ya wanachama pamoja na kuongeza uhuru wa masoko ya bidhaa kwa jumiya hiyo katika masoko ya nje.
Mkutano huo unasharikisha Wizara mbalimbali ikwemo Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii,Wizara ya Viwanda na biashara,Wizara ya Chakula na Kilimo pamoja na shirika la viwango Tanzania (TBS)

Bella kuonyesha heshima kwa akina mama

Akikonga nyoyo za mashabiki waliofurika katika uwanja wa Lake Tanganyika kupitia Tamasha kubwa la Kili Music Tour mkoani Kigoma, Christian Bella amejipanga kuonyesha heshima kubwa kwa akina mama jijini Dar es Salaam.
Christian Bella aka Mzee wa Masauti ameongea na enewz kuwa ameandaa tukio hilo kubwa la Live lililobatizwa jina 'Usiku wa Nani Kama Mama litakalofanyika tarehe 29 mwezi huu, lengo kubwa la show hiyo ni ya kutoa heshima kubwa kwa akina mama ambao ndio watu muhimu katika jamii duniani.
Mfalme huyo wa masauti ameelezea kuwa show hiyo itakuwa ni Live ambapo mkali huyo amewashirikisha wasanii maarufu watakaomsindikiza stejini akiwemo Ommy Dimpoz aliyeshirikishwa katika wimbo huo, wengine watakaompa tafu live stejini ni wasanii Banana Zorro, Matonya, Cassim Mganga, Dully Sykes pamoja na bendi ya Malaika.

video:ajali ya basi la hood hii hapa

Kijana wa mtaani aliyepanda jukwaani na Miley Cyrus kupokea tuzo MTV VMAs anasakwa na polisi

Kijana wa mtaani aliyepanda jukwaani na Miley Cyrus kupokea tuzo MTV VMAs anasakwa na polisi Kijana aliyekuwa akiishi mitaani, Jesee Helt aliyepanda katika jukwaa la MTV VMAs na Miley Cyrus na kumpokelea tuzo ya video bora ya mwaka anatafutwa na polisi wa Oregon.
Kwa mujibu wa ripoti za mahakama, kijana huyo aliwahi kukamatwa na kufungwa jela siku 30 baada ya kukutwa na hatia ya makosa mbalimbali likiwemo kosa la kuingia kwenye nyumba ya bwana mmoja bila kibali mwaka 2010.
Pamoja na kifungo hicho, kijana huyo ambaye wakati huo alikuwa na umri wa miaka 18 aliwekwa chini ya kipindi cha matazamio (probation) lakini alivunja masharti baada ya kutoka.
Mahakama ilitoa kibali cha kumkamata tangu mwaka 2011 lakini hawajafanikiwa. Kijana huyo alihamia Los Angeles na kuishi mitaani huku akijaribu kutafuta kazi ya kuwa mwanamitindo.
Miley Cyrus alikutana na kijana huyo katika kituo cha vijana wadogo wanaoishi katika mazingira magumu cha ‘Hollywood homeless Center My Friend’s Place’.
Kijana huyo alipanda jukwaani kupokea tuzo ya Video bora ya mwaka hiyo akiwa na Miley Cyrus (Kumuwakilisha) na alitoa hotuba iliyowagusa wengi kuhusu kuwaangalia vijana wanaoishi katika mazingira magumu.

Video Mpya: She Came to Give It to You- Usher Feat. Nicki Minaj

Video Mpya: She Came to Give It to You- Usher Feat. Nicki Minaj
Siku mbili baada ya tuzo za MTV VMAs, Usher Raymond ameachia video ya wimbo wake ‘She Came to Give It to You’ aliyomshirikisha Nicki Minaj.
Video imeongozwa na Philip Andelman.

Kim Kardashian aigiza katika kipindi cha ucheshi 'Comedy'

Kim Kardashian aigiza katika kipindi cha ucheshi
Kim Kardashian West amekuwa mhusika kwenye kipindi cha usheshi cha 2 Broke Girls cha CBS, kitakachoruka October 27 mwaka huu.
Kim K ametangaza hatua hiyo kupitia akaunti yake ya twitter na kueleza kuwa atacheza na waigizaji wa kike ‘Beth Behrs na Kat Dennings

utabiri wa hali ya hewa

Arusha
Weather: Partly Cloudy conditions and sunny periods.
Min. Temp.: 13°C
Max. Temp.: 26°C
Sunrise: 06:38
Sunset: 18:37
Wind:
Kilimanjaro
Weather: Partly Cloudy conditions and sunny periods.
Min. Temp.: 16°C
Max. Temp.: 31°C
Sunrise: 06:36
Sunset: 18:35
Wind:
Manyara
Weather: Partly Cloudy conditions and sunny periods.
Min. Temp.: 13°C
Max. Temp.: 26°C
Sunrise: 06:38
Sunset: 18:37
Wind:
Moshi
Weather: Partly Cloudy conditions and sunny periods.
Min. Temp.: 18°C
Max. Temp.: 30°C
Sunrise: 06:35
Sunset: 18:34
Wind:
Dar es Salaam
Weather: Partly Cloudy conditions and sunny periods.
Min. Temp.: 20°C
Max. Temp.: 32°C
Sunrise: 06:30
Sunset: 18:22
Wind: South-Easterly at 30km/hr
Morogoro
Weather: Partly Cloudy conditions and sunny periods.
Min. Temp.: 16°C
Max. Temp.: 29°C
Sunrise: 06:37
Sunset: 18:29
Wind:
Pemba
Weather: Partly Cloudy conditions, rain showers over few areas and sunny periods.
Min. Temp.: 24°C
Max. Temp.: 29°C
Sunrise: 06:29
Sunset: 18:25
Wind: South-Easterly at 30km/hr
Pwani/Coast
Weather: Partly Cloudy conditions and sunny periods.
Min. Temp.: 20°C
Max. Temp.: 32°C
Sunrise: 06:29
Sunset: 18:25
Wind: South-Easterly at 30km/hr
Tanga
Weather: Partly Cloudy conditions, rain showers over few areas and sunny periods.
Min. Temp.: 21°C
Max. Temp.: 30°C
Sunrise: 06:29
Sunset: 18:25
Wind: South-Easterly at 30km/hr
Zanzibar
Weather: Partly Cloudy conditions, rain showers over few areas and sunny periods.
Min. Temp.: 23°C
Max. Temp.: 30°C
Sunrise: 06:30
Sunset: 18:22
Wind: South-Easterly at 30km/hr

Paper work inakuja ya T.I

Album ya tisa ya mtu mzima T.i paper working anakaribia kutoka na usiku wa kuamķia leo ameachia cover art ya album hiyo na hii itajumuisha ngoma zote mpya na hit pia na kwenye insta amepost akiwa studio akimalizia ngoma na luda stay tune

Monday, August 25, 2014

Wambura apanda cheyo TFF

Kutoka kwenye mkutano na wandishi wa habari muda huu TFF imefanya mabadiliko kwa kumtoa wambura kuwa msemaji mpaka mkurugenzi wa mashindano ni updare toka Tff usikose kili break fast show leo.powerd by tigo

Ushirikiano wa TGNP na wanahabari huu hapa

TGNP mtandao chini ya uratibu chama cha waandishi wa habari wanawake TAMWA ikichirikiana na chama cha wanasheria zanzibar ZEFALA na chama cha wanasheria TAWLA wanatekeleza mradi wa miaka miwili 2012-2014 unaoitwa usawa wa jinsia na uwezeshaji wa wanawake gewe11.

Ngoma ya ben paul ipo hapa

Pakua wimbo Rasmi wa "BenPol-Twaendana" HAPA https://mkito.com/song/benpol-twaendana/2376 follow @iambenpol @defxtro @noizmekah

Sunday, August 24, 2014

Dancer wa Nicki Minaj ang'atwa na nyoka aina ya anaconda wakati wa mazoezi ya kucheza wimbo wa 'Anaconda'

Dancer wa Nicki Minaj angMmoja kati ya wachezaji wa Nicki Minaj ameng’atwa na nyoka aina ya Anaconda mwenye urefu wa futi 6 wakati wakifanya mazoezi ya kwa ajili ya show ya tuzo za video za MTV (MTV Video Music Awards).
Kwa mujibu wa TMZ, Nicki Minaj alikuwa jukwaani na dancers wake wakifanya mazoezi ya kucheza hit ya ‘Anaconda’ ambapo dancer mmoja wa kike aling’atwa na moja kati ya nyoka waliokuwa wamewekwa kwenye kontena kwa ajili ya kufanyia mazoezi
Inaelezwa kuwa nyoka hao aina ya Anaconda hawakuwa na sumu lakini wana uwezo wa kusambaza bacteria ambao husababisha matatizo kiafya.
Msichana huyo alipelekwa hospitalini kupata matibabu.
Haijulikani kama bado Nicki Minaj atapanda na nyoka hao katika jukwaa la MTV VMAs, Jumapili .
Nicki hatakuwa mwimbaji wa kwanza kupanda na nyoka kwenye tuzo hizo, mwaka 2001 Britney Spears alipanda na joka kubwa wakati anaimba ‘I’m A Slave 4 U’.

Saturday, August 23, 2014

Chibow afungua duka la nguo

Msani wa mziki wa kizazi kipya tanzania chiibow amefunguka kwa thade expensive leo kuwa kwasasa mziki una lipa na ameamua kufungua duka la nguo alilolipa jina la mtoto wa pwani classic wear.
Kwa mujibu wa chibow mwenyewe amesema kuwa duka hilo ni maalumu kwa nguo zote na lipo maeneo ya moshi bar gongo la mboto jijini dar na ni kwakuwa anapenda kuvaa na kwakuwa anatakuwa fanya wengine wapendeze pia.
Chibow amekuwa mmoja kati ya wasanii wa mziki wa bongo walio kwenye biashara ya nguo kama vile roma, izzo b na wengine pia.

Wachina wasamaki wa magufuli nikuupdate

Baada ya kusota rumande kwa miaka mitano hatimaye raia wawili wa China waliokuwa wanakabiliwa na kesi ya kuvua samaki katika Ukanda wa Kiuchumi wa Bahari ya Tanzania bila kibali wameachiwa huru katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Aidha, mahakama imeamuru washitakiwa warudishiwe mali zao, ikiwemo meli iliyotumika kufanya uvuvi huo ikiwezekana na samaki walikutwa nao pamoja na hati zao za kusafiria. Kwa mara ya kwanza, walishitakiwa watu 35 kutoka mataifa tofauti ya Bara la Asia, kama vile China, Ufilipino, Vietnam na wawili raia wa Kenya, walikamatwa Machi 8, mwaka 2009 wakivua na walikutwa na tani 293 za samaki wakati huo, Dk John Magufuli akiwa Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, hali iliyochangia samaki waliokamatwa kuitwa wa 'Magufuli’ hasa baada ya serikali kuamua kutaifisha meli na pia kugawa samaki kwa wananchi, vyuo na taasisi nyingine za umma. Kati ya washitakiwa hao, 35 waliachiwa huru na wawili kutiwa hatiani. Hakimu Mfawidhi Isaya Arufani aliwaachia huru washitakiwa hao jana baada ya Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kuwasilisha hati ya kutokuwa na nia ya kuendelea na mashtaka hayo. Washitakiwa hao ni nahodha wa meli ya Tawaliq 1 iliyotumika kufanya uvuvi huo, Hsu Chin Tai na wakala wa meli hiyo, Zhao Hanquing. Awali Wakili wa Serikali Mwandamizi Prosper Mwangamila akisaidiana na Wakili Tumaini Kweka, alidai kuwa, DPP amewasilisha hati ya kuwaondolea mashitaka washitakiwa hao kwa kuwa hana nia ya kuendelea kuwashitaki na kuomba ipokelewe mahakamani. Wakili wa Utetezi Kapteni Ibrahim Mapinduzi aliiomba mahakama washitakiwa warudishiwe mali zao vikiwemo vielelezo vinavyoshikiliwa Mahakama Kuu ambayo ni meli waliyokamatwa nayo. Wakili Mwangamila alidai washitakiwa watapewa mali zao isipokuwa meli mpaka watakapothibitisha ni wamiliki wa meli hiyo. Awali washitakiwa hao walikuwa wakitumikia kifungo cha miaka 30 jela tangu Februari 23 mwaka 2012 baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kuwatia hatiani kwa kufanya uvuvi haramu. Machi 28 mwaka huu Mahakama ya Rufani iliwaachia huru baada ya kushinda rufaa yao ya kupinga adhabu ya kifungo hicho au kulipa faini ya Sh bilioni 20 iliyotolewa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam. Hata hivyo washitakiwa walikamatwa tena na Machi 31 walifikishwa katika Mahakama ya Kisutu na kusomewa upya mashitaka yao.HabariLeo - Wachina wa 'Samaki wa Magufuli’ waachiwa

Friday, August 22, 2014

Ushauri wa madaktari kwa wizara ya afya


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii nchini Tanzania Dkt Seif Rashid
Madaktari wa magonjwa ya binadamu, wameishauri wizara ya afya na ustawi wa jamii kuhakikisha inapanua wigo wa uboreshaji wa huduma za maabara ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira mazuri kwa sekta binafsi.
Akizungumza katika majadiliano ya madaktari wa mkoa wa Arusha mtaalamu wa magonjwa ya kina mama Dkt. Frank Msuya amesema wananchi wengi hususani wa kipato cha chini wamekuwa wakikosa tiba sahihi kutokana na kukosa vipimo vya uhakika vinavyoonesha ugonjwa.
Kwa upande wake mtaalamu wa maabara kutoka maabara ya Lancet iliyozinduliwa hivi karibuni jijini Arusha Bw. Ahmed Calleb amesema siku zote utendaji kazi bora wa daktari unafanikishwa na majibu sahihi ya vipimo vya mgonjwa.
 
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt Seif Rashid

Video: Kionjo cha video mpya ya wimbo Profesa Jay 'Kipi Sijasikia'

Video: Kionjo cha video mpya ya wimbo Profesa Jay Profesa Jay anajiandaa kuachia video ya wimbo wake ‘Kipi Sijasikia’ aliomshirikisha Diamond Platinumz.  msanii huyo mkongwe ameachia kionjo cha video hiyo iliyoongozwa na Adam Juma wa Visual Lab. Kiangalie hapa

Malkia kuja rasmi na 'Ogopa Kopaz'


                             msanii wa Mipasho Khadija Kopa akiwa na wanawe
Malkia huyo gwiji wa miondoko hiyo nchini amesema kundi hilo jipya litaufikisha muziki wa Taarab hapa Bongo katika ngazi nyingine ya juu kabisa. Khadija akiwa kama msanii msomi, kundi lake la Ogopa Kopaz litaanza kazi kwa kasi likitanguliwa na ujio wa albam zake mbili 'Mama Mukubwa' na 'Kantangaze'.

Video ya Nicki Minaj 'Anaconda' yavunja rekodi ya Vevo

rekodi ya Vevo kwa kuangaliwa zaidi ya mara Milioni 19.6 ndani ya saa 24 tangu ilipowekwa.
Video hii imeipiku video ya Miley Cyrus ‘Wrecking Ball’ iliyokuwa ikishika nafasi ya kwanza tangu mwaka 2013 kwa kuangaliwa zaidi ya mara 19.3 ndani ya siku moja ilipoachiwa.
Hadi sasa Anaconda imeshaangaliwa zaidi ya mara milioni 38.5 tangu ilipotoka rasmi August 19

50 Cent kuchangia $750,000 kama Mayweather ataweza kusoma ukurasa mmoja wa 'Harry Potter'

50 Cent kuchangia $750,000 kama Mayweather ataweza kusoma ukurasa mmoja wa
50 Cent amekuja kivingine katika challenge ya kuchangia matibabu na elimu kuhusu ALS kwa kumtaka bondia Floyd Mayweather kusoma kwa sauti bila kusita ukurasa mmoja tu ya riwaya ya Harry Potter.
Rapper huyo amepost katika ukurasa wake wa Facebok kipande cha video akieleza challenge yake kwa Floyd akidai endapo ataweza basi yeye atachangia kiasi cha $750,000 kwenda katika taasisi itakayopendekezwa na bondia huyo.
“This is a special ASL-ELS challenge for you, Floyd! If you can read one full page of a Harry Potter book, I'll give $750,000 to whatever charitable organization you want to.” ALisema kabla ya kurusha mbali ndoo ya barafu. “F**k the bucket of ice, man.”
Baadae aliandika caption kwenye video hiyo akitaka kumfafanulia bondia huyo kinachotakiwa.
“Floyd will you except my ALS/ESL CHALLENGE: I will donate $750k to a charity of your choice, If you can read a full page out of a Harry Potter book out loud without starting and stopping or f**king up. lmao.”

Picha: Familia ya Kichina yakosolewa kwa kumgeuza mtoto mfano wa 'msosi'

Picha: Familia ya Kichina yakosolewa kwa kumgeuza mtoto mfano wa
Familia ya kichina imekosolewa vikali na watu mbalimbali wanaopigania haki za watoto baada ya kuonesha picha ya mtoto wao mchanga akiwa katikati ya misosi huku akiwekewa mboga kama sehemu ya salad.
Mama yake mzazi, Qu Quan amesema kuwa wao walifanya kwa utani na walikuwa wakicheka sana kumuona mtoto akijaribu kuamka kutoka kwenye bakuli hilo huku akishindwa na kuendelea kulia na kisha wakamtoa.
Hata hivyo, sio wote waliowakosoa seriously, wengine walitania “Chinese people are capable of anything. The baby could be one of the menu.”

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...